Jamhuri ya Muungano wa Tanzania

Taasisi ya Taaluma ya Wanyamapori Pasiansi

Astashahada ya Awali ya Uongozaji Watalii na Usalama

Kozi ya Astashahada ya Awali ya Uongozaji Watalii na Usalama, imeandaliwa kwa ajili ya kuwaandaa vijana waliohitimu kidato cha nne kuwa Waongoza Watalii wenye Kuzingatia mbinu za Usalama katika shughuli zao za kila siku katika Taasisi za Serikali, Mashirika binafsi, Jumuiya za Hifadhi za Vijiji, Makampuni ya Utalii, Uhifadhi na Uwindaji na Mashirika ya Kimataifa. Mafunzo haya yanatolewa kwa kipindi cha mwaka mmoja na yatamuwezesha mhitimu kufanya kazi za kawaida za kila siku katika Taasisi, Kampuni na Mashirika tajwa. Kazi hizo ni kama ifuatavyo:

  • Kuongoza Watalii katika vivutio vya aina mbalimbali Tanzania,
  • Kuelezea tafsiri ya vivutio kwa lugha za Kiswahili na kimataifa,
  • Kuwapa taarifa sahihi watalii katika kivutio husika,
  • Kukusanya na kuweka takwimu za watalii na safari za kitalii,
  • Kujibu malalamiko kutoka kwa Watalii,
  • Kusimamia miundo mbinu ya eneo la utalii,
  • Kutoa ushauri wa kitaalamu kwa Taasisi, Shirika na Kampuni iliyomwajiri,
  • Kutunza kumbukumbu za vitabu/majalada/majarida ya kitalii,
  • kufanya kazi za ulinzi na doria katika maeneo ya ndani na nje ya eneo la kazi,

kufanya shughuli zingine za kawaida zitakazotolewa na viongozi sehemu za kazi.

Code

Module Title

Mhula

1

2

TMT 04101

Kanuni za Utalii

 

TMT 04202

Kanuni za Huduma kwa Wateja

 

TMT 04103

Misingi ya Ujuzi wa Kuongoza Watalii

 

TMT 04104

Tafsiri ya Vivutio vya Utalii vya Kibaiolojia

 

TMT 04205

Tafsiri ya Vivutio vya Utalii vya Kiutamaduni

 

TMT 04206

Misingi ya Sheria za Utalii na Uhifadhi wa Maliasili

 

TMT 04207

Misingi ya Usalama na Utalii

 

TMT 04108

Huduma ya Kwanza na Matibabu ya Dharura

 

TMT 04209

Kanuni za Ujasiliamali wa Biashara ya Utalii

 

TMT 04110

Ujuzi wa Fani ya Mawasiliano

 

TMT 04211

Mafunzo ya Awali ya Kompyuta

 

TMT 04112

Ujuzi wa Mbinu za Maisha

 

TMT 04213

Misingi ya Utengenezaji Magari

 

 

FAIDA ZA KUSOMA KOZI YA MSINGI YA UFUNDI WA UONGOZAJI WATALII NA USALAMA

  • Atafahamu kanuni za Uongozaji Utalii     - Basics of Tour Guiding Skills
  • Ataweza kutoa huduma kwa mteja kitaalamu - Customer Care Skills
  • Ataweza kutafsiri vivutio vya kibailojia na kitamaduni kwa Ufasaha – Biological and Cultural Interpretation Skills
  • Atafahamu Sheria za Utalii na Uhifadhi – Tourism and Conservation Laws
  • Atafahamu Misingi ya Usalama na kutoa huduma ya Kwanza kwa Watalii – Tourism Safety, First aid and Emergency Care Skills
  • Atapata Ujuzi wa Kutumia Tarakilishi – Computer Skills
  • Atajifunza Ufundi wa Magari – Basics of Motor Vehicle Maintanance

NYOTE MNAKARIBISHWA