Jamhuri ya Muungano wa Tanzania

Taasisi ya Taaluma ya Wanyamapori Pasiansi

Habari
TANGAZO LA WALIOCHAGULIWA KUJIUNGA NA MAFUNZO YA TAASISI MACHI 2024

Mkuu wa Taasisi ya Taaluma ya Wanyamapori Pasiansi, Mwanza anapenda kuwajulisha wafuatao kuwa wamechaguliwa kujiunga na kozi ya Astashahada ya Awali ya Usimamizi wa Wanyamapori na Hima Sheria (BTCWLE) katika udahili wa Machi 2024 kwa mwaka wa masomo 2024/2025. Waliochaguliwa wanatakiwa kuripoti Jumatatu tarehe 25 Machi 2024 hadi tarehe 27 Machi 2024.

 

TAFADHALI ZINGATIA: Mafunzo ya Taasisi ya Taaluma ya Wanyamapori yanafuata mfumo wa Jeshi Usu (paramilitary). Wote waliochaguliwa wanawajibika kuchukua fomu ya kupimwa afya zao katika Hospitali ya Wilaya, Mkoa au Rufaa. Kutokuzingatia hilo kutakuondolea sifa ya kujiunga katika mafunzo.

BONYEZA HAPA KUPAKUA MAJINA YA WALIOCHAGULIWA MACHI 2024

BONYEZA HAPA KUPAKUA FOMU YA MAELEZO YA KUJIUNGA NA KOZI YA BTCWLE Na. 60

BONYEZA HAPA KUPAKUA CONTROL NUMBER ZA KULIPIA ADA

BONYEZA HAPA KUPATA ORODHA YA VIFAA NA BEI VINAVYOPATIKANA KATIKA DUKA LA TAASISI

 

                                                              Imetolewa na;

Mkuu wa Taasisi

15 Machi 2024